Yawezekana
umewahi kusoma au kusikia historia za makabila mbalimabli, hasa ya Wasukuma na
Wanyamwezi, lakini huenda hukupata kusikia habari ya Ng’wanamalundi kwa undani
zaidi. Wapo wengi wamejaribu kumsimulia lakini si kwa undani zaidi.
Kwa
wakristo, ukisoma habari za Yesu utaona maajabu aliyofanya yakiwemo ya kutembea
juu ya maji, kuzuia dhoruba ya mawimvi ya bahari na yakamtii, n.k Ng’wanamalundi
nae amefanya maajabu yanayofanana na hayo likiwemo ya kutenganisha bahari
kukawa na barabara na kupita akitembea kama nchi kavu, kulima viazi asubuhi na
jioni akaenda kuvuna, kukausha miti n.k. Kwa Undani zaidi soma habari zake
katika kitabu hiki.
Utangulizi
Ng’wanamalundi alizaliwa katika ukoo wa kawaida
kijijini Mwakubunga Nera wilaya ya Kwimba mkoa wa Mwanza. Makuzi yake yalikuwa
chini ya wazazi wake mzee Bugomola na Ngolo Igulu hapo kijijini. Ng’wanamalundi anaitwa mtoto wa dawa kwa sababu baba
na mama yake huko nyuma uzazi ulikuwa wa shida shida hivo kupata mtoto ilifika
mahala ikawa ni tatizo kubwa. Mara baada ya baba yake kuhangaika sana mwisho
aliamua aende kwa Mganga wa jadi. Alipofika kwa mganga huyu, mzee Bugomola
alipewa maelezo ya masharti na Mganga wa Jadi kuwa akubali kufa mara baada ya mtoto
kuzaliwa. Mganga wa jadi ali mueleza mzee Bugomola kuwa atapewa dawa ataitumia
na watapata mtoto wa kiume mwenye maajabu sana. Hivyo mzee Bugomola
alikubaliana na masharti ya maganga wa jadi na akapewa dawa akatumie. Inaelezwa
kuwa mzee Bugomola amefariki mara baada ya Mtoto kuzaliwa na mtoto alipewa jina
la Igulu.
Alipokua na kufikia makamo alianza kucheza ngoma. Alipofikia umri wa miaka ishirini aliondoka nyumbani pamoja na vijana wenzake wawili wa pale kijijini kwenda kwa bibi kizee aliyekuwa maarufu sana ili kupata dawa ya 'Nsamba'. Nsamba ni dawa ya kisukuma (Nitailezea baadae). Dawa hii ilimfanya awe mcheza ngoma mashuhuri sana. Hata hivo maandiko…….
Alipokua na kufikia makamo alianza kucheza ngoma. Alipofikia umri wa miaka ishirini aliondoka nyumbani pamoja na vijana wenzake wawili wa pale kijijini kwenda kwa bibi kizee aliyekuwa maarufu sana ili kupata dawa ya 'Nsamba'. Nsamba ni dawa ya kisukuma (Nitailezea baadae). Dawa hii ilimfanya awe mcheza ngoma mashuhuri sana. Hata hivo maandiko…….
Email: masele97@yahoo.com
Simu: 0783-846901