Je Wajua maana ya Neno "Wasukuma"?
Kabila la wasukuma ni changa kuliko makabila yote ya
Tanzania bara maana historia ya kabila hili haiendi nyuma zaidi ya mwaka 1500
ambapo miaka hiyo makabila mengi ya Tanzania yalikuwa yanatambulika.
Katika
Kitabu cha jumuiya ya watemi wa kisukuma kiliandiaka kuwa miaka ya 1550, kabila
la wasukuma ndio lilianza kujikusanya na kutengeneza makao maalumu. Utafiti
unaonesha kuwa kihistolia kabila hili halikutoka nje ya Tanzania (primary
immagrant) kama ilivyo kwa makabila mengine. Kabila hili lilitokana na
mwingiliano wa kuoana (intermarriage) baina ya makabila yaliyokuwa yakitokea
nje na kuingia Tanzania yakiambaa mashariki na magharibi mwa ziwa victoria. Mpaka
katikati mwa karne ya 14, iliingia misafara ya wahamiaji wengi kutoka Uganda, Kenya,
Sudani, Rwanda, na Congo, wakatua kuzunguka ziwa victoria kuendesha shuguli za
uwindaji na uvuvi. Wakaanza kuoana na kuanzisha lugha tofauti kulingana na
mazingira. Mfano Misafara iliyotoka Kenya, Sudani na Ethiopia ilitua kaskazini
mashariki mwa ziwa victoria, mchanganyiko wa misafara hii, ilitengeneza lugha
ya Wazanaki, Washashi, Wajita, Wakulya. Misafara kutoka Uganda, Rwanda,
Burundi na Congo walitua mgharibi mwa ziwa victoria huku wakizalisha makabila
ya Balongo (bakamba au wafua vyuma), Bashi (wawindaji), Bashoma, Bazinza,
Washubi. Miaka ya 1400 Makabila ya Magharibi mwa ziwa (yaani Balongo, Bashoma,
Bazinza, Bashi, na Washubi) walianzisha biashara ya vyuma vya kilimo na
uwindaji wakaanza kuwauzia watu wa Mashariki na kusini mwa Ziwa (Wanyamwezi,
Wajita, Washasi, Wazanaki Na Wakulya) biashara hii iliwafanya waanze kuoana na
kuzaliana. Mwingiliano (intermarriage) baina ya makabila haya yenye lugha na
tamaduni tafauti, baada ya miaka mingi kuliibua Lugha mpya tofuati ikiwa na
mchanganyiko wa misamiati na rahaja mbalimbali kutoka lugha mama (Vernacular Language).
Lugha hii ilikua kwa kasi sana kwani hawa watu
walikuwa na uwezo wa kuzaliana sana kuliko saidiwa na wingi wa vyakula, samaki
na wanyama pori. Mwishoni mwa karne ya 15 watu wa lugha hii ngeni walianza
kujikusanya makundi makundi na kuanzisha makazi ya kudumu maeneo mbali mabli
kuzunguka ziwa victoria na mapori ya kaskazini mashariki mwa Tanzania. Kabila
hili badae lilitambulikana kwa majina tofauti tofauti kulingana na mahali.
Mfano Wajita waliwaita WAGWE na Washashi waliwaita WAKLITI. Mnamo mwaka 1550
watu hawa walianza kuambaa kusini (dakama
kwa kisukuma) ambapo.....
Soma Kitabu cha Historia ya Wasukuna Na Ng'wanamalundi kwa undani Zaidi.